Na: Mwanakheri Ally
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Dr. Japhet Simeo amewahamasisha Wananchi wa Kijiji cha
Chimbila 'A' na Manokwe kuanza taratibu za ujenzi wa boma za Zahanati kama
walivyoagizwa na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa wakati wa ziara yake Wilayani hapo iliyofanyika mwezi mliopita.
Dr. Simeo aliwaambia Wanakijiji wa Chimbila 'A' wajitahidi waanze ujenzi wa Zahanati kwa nguvu zao kwani kuanza kwao kwa ujenzi
itawasaidia kupata msaada kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa na sikutegemea kusubiria Serikali
ije iwaanzishie ujenzi.
Hayo aliyaeleza wakati wa mkutano wa uhamasishaji wa ujenzi wa Zahanati
uliofanyika katika ofisi ya Serikali ya kijiji cha Chimbila 'A'.
Mganga Mkuu aliwaambia kama watajitahidi kuwa na kasi katika
suala la ujenzi wa Zahanati basi mwezi wa Nane mwaka 2017 Zahanati hiyo itaweza
kufunguliwa kama watakuwa wamemaliza ujenzi.
Aidha, Dr. Simeo alitumia nafasi hiyo kuwapa pole Wanakijiji wa Chimbila 'A' kwa kuuguliwa na Diwani wao Daniel Mtawa na kuwataka kuwa na moyo wa uvumilivu kwa
kipindi hiki kigumu kwao.
“kuweni na uvumilivu kwani hiki nikipindi kigumu kwenu ila
zidisheni dua na maombi kwani Mh Diwani anaendelea kupata matibabu katika
Hospitali ya Muhimbili” alisema.
|
Mganga Mkuu Dokta Japhet Simeo akiwa katika kijiji cha Chimbila 'A' katika mkutano wa Kijiji wa kuhamashisha ujenzi wa Zahanati. |
|
Mjumbe wa SerIkali ya Kijiji cha Chimbila 'A' akiwa anatoa mchango wake wa mawazo ni vipi wataweza kujenga Zahanati hiyo |
|
Wanakijiji wa Chimbila 'A' wakiwa wanamsikiliza kwa umakini Mganga Mkuu |
|
Wananchi wa Chimbiila A wakiwa katika mkutano wa kijiji wa uhamasishaji wa ujenzi wa Zahanati |
|
Viongozi wa Kijiji cha Chimbila wakiwa wanaelekea kwenye eneo lililochaguliwa na wananchi kwa ujenzi wa zahanati |
| | | | | |
| | | | | Mganga
Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa akiwa anaongea na viongozi wa Serikali ya
Kijiji cha Manokwe wakati wa kukagua eneo litakalojengwa zahanati katika
kijiji hicho | | | | | | | | | | | | | | |
|
|
|
Eneo la Kijiji cha Chimbila A linalotegemewa kujengwa Zahanati |
|
Mganga
Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa akiwa anaongea na viongozi wa Serikali ya
Kijiji cha Chimbila A wakati wa kukagua eneo litakalojengwa zahanati katika
kijiji hiko |
|
Viongozi wa Serikali ya kijiji Manokwe wakiwa wanaangalia eneo la kufanya ujenzi wa Zahanati kijijini hapo |
|
Mtendaji wa Kijiji wa Chimbila A akiwa na Wajumbe wa kijiji hiko wakimuonesha Mganga Mkuu eneo wanalotaka kujenga zahanati |
|
Eneo la Kijiji cha Chimbila A linalotegemewa kujengwa Zahanati lenye ukubwa wa zaidi ya ekari 4 |
|
Mganga Mkuu akiwa na viongozi wa kijiji cha Chimbila wakiwa wanaangalia eneo la ujenzi wa Zahanati huku mganga mkuu akiwa anawapa mbinum za kuanzisha ujenzi |