Sunday 8 October 2017

Mhe, Kigwangala Ameagiza Kukarabatiwa Kwa Vyumba Vya Upasuaji Katika Vituo Vya Afya Ruangwa

NA MWANDISHI WETU

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Hamisi Kigwangala ameuangiza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kumalizia chumba cha upasuaji cha Kituo cha Afya Mandawa kwa muda wa mwezi mmoja kuanzia 06/10/2017.

Pia aliagiza kumaliziwa kwa chumba cha upasuaji cha Kituo cha Afya Mbekenyera kwa muda wa miezi 3 kwa kubadilisha vyumba vilivyokusudiwaa kwa wodi za wazazi kuwa jengo la upasuaji.

Mhe, Naibu Waziri aliyasema haya wakati wa ziara yake ya kikazi aliyoifanya katika Wilaya ya Ruangwa tarehe 06/10/2017 alipotembelea vituoa vya Afya vilivyopo katika Wilaya hiyo ambavyo ni Kituo cha Afya cha Luchelegwa, Nkowe, Mbekenyera, na Mandawa pia alipata nafasi ya kutembelea zahanati ya Nandagala.

Naibu Waziri alisema katika utawala huu wa awamu ya tano ni lazima kila kituo cha Afya kiwe na chumba cha upasuaji, hivyo ni bora kuwa na chumba kidogo kuliko kukosekana kabisa  chumba cha upasuaji.

“Mhe Mkuu wa Wilaya wewe hapa hauna vituo vya Afya una zahanati zenye majengo mengi vituo hivi vinamapungufu mengi ila ni lazima kuwepo na vyumba vya upasuaji ili kusaidia na kukidhi mahitaji ya wananchi” alisema Kigwangala.

Pia Naibu Waziri Kigwangala alimtaka Mkurugenzi wa Halmashauri kuwezesha kupatikana kwa maji katika vituo vyote vya afya vilivyopo katika wilaya hiyo alisisitiza kupatikana kwa maji katika hospitali kubwa na kubadilisha mabomba yaliyopo sasa katika vituo na hospitali ya wilaya.

Vile vile Naibu Waziri Kigagwala aliutaka uongozi wa hospital kufanya mchakato wa kufunga mfumo wa kielektroniki(GoT HOMIS) kwenye maeneo mengine na si kuishia mapokezi tu kama ilivyo sasa ili kudhibiti vyema mapato yanayoingia katika vituo hivyo na Hospitali ya Wilaya.

Naye Mganga Mkuu wa Wilaya Dr, Japhet Simeo alimuomba Mhe, Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii na Jinsia Dr, Kigagwala awasaidie  upatikanaji wa ramani rahisi zenye gharama nafuu kwa wananchi.
Dr, Simeo alisema ramani zilizoletwa Halmashauri zina na makadirio makubwa ya fedha ambayo kwa uhalisia utekelezaji wake unakuwa ni mgumu kwa wananchi.

“Sera ya sasa inawataka wananchi waanze kufanya shughuli za kimaendeleo kama ujenzi wa Zahanati mpaka kwenye boma alafu Halmashauri zimalizie ila kwa makisio ya fedha zinazokuwa zinaletwa inakuwa ngumu kwa wananchi kutekeleza Mhe, Kigagwala naomba suala hili ukatusaidie lipatiwe ufumbuzi kutokana na hali za wananchi wetu”alisema Dr, Simeo
kushoto) Mhe, Naibu Waziri Kigwagala akiwasili katika kituo cha Afya cha Luchelegwa baada ya kutoka Lindi Mjini.(kulia) Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mhe, Joseph Mkirikiti

Afisa Tabibu Msaidizi wa Kituo cha Afya Luchelegwa Godfrey Kalembo akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Dr, Kigwagala alipotembelea kituo cha Afya Luchelegwa

Mganga Mkuu wa Wilaya Dr, Japhet Simeo akiwa anatoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Afya Dr, Kigwagala katika kituo cha Afya Luchelegwa

(kushoto)Mheshimiwa Diwani wa Kata ya Nandagala Chikongwe akiwa anateta jambo na Mhe, Mkuu wa Wilaya Joseph Mkirikiti

Naibu Waziri Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto akisaini kitabu cha wageni katika zahanati ya Nandagala alipofanya ziara yake ya kikazi katika Wilaya hiyo

Wambele) Mganga Mkuu wa Wilaya Dr, Japhet Simeo akimuongoza Mhe Naibu Waziri alipokuwa anatoka kukagua jengo la wodi ya kina mama


Mhe, Kigwagala akikagua ujenzi wa chumba cha kujifungulia kina mama na chumba cha upasuaji katika zahanati ya nandagala unaoendelea kujengwa

(wakatika) Mhe Diwani wa kata ya Nandagala akimsindikiza Mhe Naibu waziri alipomaliza kukagua majengo katika zahanati ya nandagala

moja ya Jengo la wodi ya kina baba na kina mama katika zahanati ya Nandagala

(kushoto)Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Joseph Mkirikiti na kulia ni Naibu waziri wa Afya akisaini kitabu cha wageni katika kituo cha afya Nkowe

Mhe, Kingwagala akikagua chuma cha kujifungulia kina mama katika kituo cha Afya Nkowe

Naibu Waziri akielekea kukagua majengo yaliyopo katika Kituo cha Afya Nkowe alipofanya Ziara yake katika Wilaya ya Ruangwa

Naibu Waziri wa Afya Dr, Kigwagala akiwaaga wauguzi wa kituo cha Afya Nkowe baada ya kumaliza kukagaua miundombinu katika kituo hiko

Naibu Waziri Kigwagala akisalimiana na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Ruangwa Dr, Regan alipotembelea hospital hiyo

Naibu Waziri akiongea na  Fundi sanifu Maabara alipotembelea maabara ya Hospitali ya Wilaya

Mganga Mkuu wa Wilaya Dr, Simeo akimuonesha Naibu Waziri wa Afya Kigwagala taa ya chumba cha upasuaji kuthibitisha kama inafanya kazi


Dr, Simeo akimuona Naibu Wzairi jengo lilalotegemewa kuwa chumba cha upasuaji katika kituo cha Afya Mbekenyera

Mhe, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia wazee na Watoto chumba kitakachofanywa kuwa chumba cha upasuaji