Wednesday 19 July 2017

Kamati Ya Fedha, Uongozi na Mipango Imetembelea Miradi ya Maendeleo 17/07.2017



Na Mwandishi Wetu

Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango imefanya  Ziara ya kutembelea   na Kukagua  Miradi ya Maendeleo ya Halmashauri ya Wilaya ikiwa ni utekelezaji wake kila robo ya mwaka. 

  Kamati hiii iligawanyika katika makundi mawili kundi A na B makundi hayo yalifanya ziara hiyo siku ya tarehe 17/7/2017 kundi A liliongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe Kambona, na Kundi B liLiongozwa na Mhe Mwenyekiti wa Kamati Rashidi Nakumbya akiambatana na wajumbe.

Kamati ilitembelea Miradi 9 ambayo ni Mradi wa kuona shule ya sekondari Kassim Majaliwa, kata ya  Nachingwea, Kisima cha Maji, Mkanjiro, Ujenzi wa Vyoo, Mabweni na Madarasa, Nkowe Sekondari, Kisima cha Maji Namakuku, ,Kuona Ujenzi wa Zahanati ya Mibure, Mibure, kuona ujenzi wa Vyumba vya Madarasa Mnacho Sekondari, Ujenzi wa Nyumba ya Mwalimu Ndandawale, ujenzi wa jengo la Utawala(Hawa Mchopa).

Kaimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Kassim Majaliwa akitoa taarifa kwa wanakamati ya Fedha, Uongozi na Mipango baada ya kutembelea shule hapo

Mwenyekiti wa Kamati Rashidi Nakumbya akiangalia uiamala wa madirisha wakati wa ziara ya kamati ya Fedha


Serikali ya kijiji cha Makanjiro pamoja na wajumbe wa Kamati wakiangalia mradi wa kisima kijijini hapo

Mhandisi wa Maji Kabange akiwa anatoa maelezo ya mradi Makanjiro

Mwenyekiti wa Kamati akiwa na wajumbe akikagua matundu ya vyoo katika shule ya sekondari Nkowe


Wanakamati ya Fedha, Uongozi na Mipango wakiwa wanaangalia mashimo ya choo yaliyojengwa shuleni Nkowe

Mwenyekiti wa Halmashauri Rashidi Nakumbya akikagua mradi wa bweni ulipo katika shule ya sekondari Nkowe, Mabweni hayo yanategemewa yawe ya kidato cha tano

Mkuu wa Shule ya Nkowe Maliki Ahmed akiwa anatoa maelezo ya mradi kwa waheshimiwa Madiwani


Bweni la wasichana linalojengwa katika shule ya Nkowe kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha tano mwakani




Vyumba vya darasa katika shule ya sekondari Mnacho mradi huu umekamilika na wanafunzi wameishaanza kufaidika nao


Katikati)Mwenyekiti wa kamati Rashidi Nakumbiya akiwa anasikiliza taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Nandawale

Jengo la Utawala katika shule ya sekondari Mnacho lilioanzwa kujengwa kwa nguvu za wananchi na Halmashauri kusaidia nguvu hizo


Chumba cha Darasa kinachojengwa shule ya Sekondari Hawa Mchopa