Wednesday 28 December 2016

WAZIRI MKUU MAJALIWA AWAONDOA HOFU WANANCHI WA RUANGWA KUHUSU KUPATIKANA KWA MAJI SAFI NA SALAMA

Na Mwanakheri Ally

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amewataka Wananchi wa Wilaya ya Ruangwa kuwa wavumilivu na wenye subira katika suala la kupatikana kwa maji safi na salama katika kila Kijiji kilichokuwa ndani ya Wilaya hiyo, kwani anafanya jitihada za kila namna ili kuweza kumaliza changamoto hiyo.

Alisema ndani ya Uongozi wake wa miaka mitano hii ya mwanzoni anataka kuhakikisha anakabiliana na kumaliza changamoto ya Umeme na Maji katika Wilaya ya Ruangwa, kwani ameshaanza mikakati ya kutafuta Wafadhili watakaowasaidia kuchimba visima virefu na kupima maji kama ni salama kwa matumizi ya Binaadamu.

Waziri mkuu ameyasema hayo wakati akizungumza wa Wananchi wa kijiji cha Chimbila A, Manokwe, Ng'au, na Nadagala wakati wa Ziara yake aliyoifanya ndani ya Wilaya ya Ruangwa siku ya Tarehe 27 mwezi Desemba 2016



Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Lindi Godfrey Zambi mara alipowasili katika uwanja wa ndege wa Nachingwea kwa ajili ya Ziara ya Kikazi katika Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Lindi Mohammed Mtopa

Waziri Mkuu akisalimiana na Mkurugenzi wa Nachingwea{DED} Bakari Mohamedi Bakari

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Mkewe Mery Majaliwa wakifurahia ngoma ya kikosi cha JKT 843KJ kilichopo Nachingwea ambacho kilikuwepo wakati wa mapokezi ya Waziri Mkuu