Thursday 20 July 2017

Mhe,Mnunduma: Amewataka wanufaika wa Mpango wa Tasaf III Kuzitumia Fedha Hizo Kwa Shughuli Za Kiuchumi

Na Mwandishi Wetu

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira Rashidi Mnunduma, amewataka wananchi wanaopokea pesa za kaya masikini wazitumie vizuri pesa hizo kwa kufanya shughuli za kiuchumi.

Alisema Mwenyekiti badala ya mtu kupokea hizo pesa na kuanza kufanya matumizi yasiyoyalazima ni vizuri mtu akawekeza katika kilimo, ufugaji wa kuku na biashara ndogondogo na hata kujenga nyumba nzuri ya kuishi.

Aliyasema hayo wakati wa ziara ya Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira baada ya kutembelea   na Kukagua  Miradi ya Maendeleo ya Halmashauri ya Wilaya ikiwa ni utekelezaji wake kila robo ya mwaka.

 
Kamati hiii iligawanyika katika makundi mawili kundi A na B makundi hayo yalifanya ziara hiyo siku ya tarehe 20/7/2017 kundi A liliongozwa na  Mwenyekiti wa Kamati Mhe , Rashidi Mnunduma na Kundi B  na wajumbe.

Kamati ilitembelea Miradi  ambayo ni Mradi wa kuona ujenzi wa barabara , kata ya  Namichiga, Ujenzi wa Zahanati, Muhuru  ,Kuona mradi wa Tasaf, kijiji cha Nahanga kata ya  Mandawa, na kuona mradi wa msitu Mchichila.

(katikati)Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira Mhe, Rashindi Nnunduma akitoa maoni yake baada ya kuona mradi wa ujenzi wa barabara namichiga


Mwenyekiti wa Kamati akiwa anaongea na wananchi wa Namichiga

Mkazi wa Kijiji cha Namichiga bwana Malengo akiwa anatoa maoni kwa wanakamati

Jengo la Zahanati kijiji cha Muhuru likiwa katika hatua za awali

(katikati) Mhe, Diwani ya Kata ya Chunyu Kambona na (kushoto) Mwenyekiti wa Kamati


Mtendaji wa kijiji cha Muhuru Awesa Juma akiwa anatoa maelezo ya Mradi kwa wanakamati(kulia)Mhe, Songea

Wataalamu kutoka Halmashauri walioambatana Waheshimiwa Madiwani



Mwenyekiti wa Kijiji cha Nahanga akisoma taarifa mbele ya wanakamati

(Katikati) Mnufaika wa mradi wa Tasaff III aliyejenga kwa fedha hizo

Mwenyekiti wa Kamati Mhe, Mnunduma akisikiliza maelezo kutoka kwa mnufaika wa mradi huo

Nyumba iliyojengwa na Hadija Lichenjera kwa fedha za Tasaf III

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mchichili akiwa anatoa maelezo ya mradi wa Msitu uliopo katika kijiji chao

Wajumbe wa Serikali ya Kijiji wakiwa katika ofisi ya kijiji

Katibu wa Kamati Zuhura Makota akimkaribisha Mwenyekiti wa Kamati

Afisa Misitu Masagya akiwa anatoa maelezo ya mradi huo  mbele ya wanakamati


Msitu uliopo katika kijiji cha Mchichila

Msitu wa Mchichila wenye hekta 450


Kamati ya Uchumi,Ujenzi na Mazingira wakiwa wanaangalia chanzo cha maji Mandawa


Jengo la jipya la Radio Ruangwa likiwa katika hatua za ukamilishaji