Thursday 4 May 2017

WALIMU WAKUU WAASWA KUTUMIA FEDHA ZA (P4R) KWA MALENGO YALIYOKUSUDIWA NA MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII ELIAS NKANE



Na Mwanakheri Ally

Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu, Afya na Maji Elias Nkane, amewataka wakuu wa shule  wanaopewa pesa kwa ajili ya kuongeza vyumba vya madarasa, chumba cha kukaa walimu na vyoo wazitumie pesa hizo kwa mahitaji yaliyokusudiwa.

Mh, Nkane Alisema pesa za lipa kulingana na matokeo (P4R) zinazopelekwa katika mashule ni nyingi hivyo zisiwatie tamaa wakuu wa shule na kuanza kuzitumia katika mipango isiyokusudiwa kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Mwenyekiti alisema hayo wakati wa ziara ya kamati ya huduma za jamii, zilipotembelea katika miradi katika kijiji cha Nachiungo, Mnacho, Chimbila A na Michenga, kamati ilitembelea shule ya msingi Nachiungo, shule ya sekondari Mnacho, mradi wa maji Michenga na kuangalia eneo la ujenzi wa zahanati katika kijiji cha Chimbila A.

Aidha Mwenyekiti aliutaka uongozi wa kijiji cha Chimbila A, kuhakikisha eneo lilotengwa kwa ajili ya ujenzi wa zahanati alivamiwi na wanakijiji kwa ajili ya shughuli za kilimo na makazi,

``Jitahidi mpaka mwezi wa 8 mwaka huu zahanati iwe imesimama hata mkiomba nguvu kutoka Halmashauri itakuwa ni rahisi kusaidiwa, serikali ya kijiji mjitahidi katika kukusanya michango`` alisema.

Naye Diwani wa Mbwemkuru aliwasisitiza viongozi vya serikali ya kijiji cha Chimbila kukusanya michango ya ujenzi wa zahanati bila kuangalia wala kupendelea ili kuweza kifikia lengo walilojiwekea.

Katika kuonesha madiwani wako karibu na wananchi wao madiwani wawili walichangia fedha za ujenzi wa zahanati hiyo  bila kuangalia kuwa siyo kata yao, vilevile mganga mkuu wa Wilaya naye alichangia fedha kwa ajili ya ujenzi wa zahanati hiyo.

Naye Mganga Mkuu wa Wilaya dr Japhet Simeo aliupongeza uongozi wa shule ya sekondari Mnacho kwa juhudi walizozionesha za kuanza ujenzi wa vyumba ya kukaa walimu ambavyo havikuwa katika mpango wa (P4R)kwani ni ubunifu mzuri ulioufanywa na uongozi wa shule hiyo.

Pia aliushauri uongozi wa kijiji cha Chambila A, kuwa na ushirikiano na jamii inayowazunguka ili kuweza kufanikisha jambo hilo, kwasababu hao ndiyo watu watakaoweza kusaidia kuendeleza au kushia njiani kwa ujenzi wa zahanati hiyo

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Nachiungo Gabrier Issa Mshiro akiwa anasoma taarifa ya mradi mbele ya wanakamati wa huduma za jamii

vyumba vya madarasa vitatu vinavyojegwa katika shule ya msingi Nachiungo

Wanakamati wakiwa wanasikiliza taarifa iliyokuwa inayosomwa na mwalimu mkuu



(Katikati)Mwenyekiti wa kamati ya Elimu, Afya na Maji akiwa anasikiliza maoni ya wajumbe(kushoto)Mganga mkuu wa Wilaya

Mganga mkuu wa Wilaya Dr Japhet Simeo akiwa anaongea baada ya kusomewa taarifa


Mwenyekiti wa kijiji cha Narung`ombe Hamisi Omari akiwa anajibu swali aliloulizwa na Mwenyekiti wa kamati

(kushoto)Diwani wa viti maalumu Paulina muya akiwa anatoa maoni yake kwa wanakamati ya ujenzi wa shule ya msingi Nachiungo

Mkuu wa shule ya sekondari Mnacho akiwa anasoma taarifa yake mbele ya kamati ya huduma za jamii ilivyofanya ziara yake katika shule hiyo

Waheshimiwa madiwani wakiwa wanasikiliza taarifa ya ujenzi kutoka kwa mkuu wa shule

Mwenyekiti wa Kamati akiwa anasikiliza taarifa kutoka kwa mkuu wa shule wa Mnacho


Ujenzi wa vyumba vya madarasa vinavyojengwa katika shule ya Mnacho

Vyumba vya madarasa vinavyojengwa kwa pesa za  (P4R) katika shule ya sekondari Mnacho

Wajumbe wa kamati wakiwa wanasikiliza taarifa

Mwenyekiti wa Kamati Elias Nkane akiwa anaongea baada ya kukagua ujenzi wa vyumba vya darasa

Mh. Nkane akiwa anaonesha wanakamati uimara wa tofali zilizojengewa choo katika shule ya sekondari mnacho

Wajumbe wa kamati wakiwa wanaangalia shimo la choo

(kushoto)Diwani wa kata ya Mbwemkuru Selemani Likuche akiwa anatoa maoni yake baada ya kuona ujenzi katika shule ya Mnacho


(katikati)Diwani wa kata ya Matambalale akiwa anatoa maoni yake baada ya kuona mradi(kulia) Kaimu Afisa Elimu wa Wilaya na(kushoto) Mganga Mkuu wa Wilaya Dr, Japhet Simeo

Mh, Diwani wa kata ya Mandawa Abdallah Nachingi akiwa anatoa ushauri wake kwa mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Mnacho baada ya kuona hali ya ujenzi

Mh, Nkane akiwa anahamasisha wanakijiji wa Chimbila A, kuanza ujenzi wa Zahanati katika kijiji hiko

Serikali ya kijiji ya Chimbila A, na kamati ya huduma za jamii wakiwa wanamsikiza Mwenyekiti wa Kamati


Mh, Diwani wa Viti maalumu akiwa anatoa ushauri kwa serikali ya kijiji cha Chimbila A, kuhusu ujenzi wa Zahanati


Waheshimiwa madiwani wakiwa wanaangalia mradi wa maji katika kijiji cha Michenga

Wajumbe wa kamati ya Elimu, Afya na Maji wakiwa katika kijiji cha michenga wakiangalia mradi wa maji

Kaimu Mtendaji wa kijiji bi, Zaituni Natunga akiwa anasoma taarifa mbele ya wanakamati



Mwenyekiti akitoa maoni yake baada ya kuuona mradi wa maji na baada ya kusomewa taarifa