Wednesday 21 December 2016

NAIBU WAZIRI POSSI AWAHIMIZA WANANCHI WA RUANGWA KUSAIDIA WATU WENYE ULEMAVU

Na: Mwanakheri Ahmed 
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu; Watu wenye ulemavu Dkt. Abdallah Possi ameitaka Halmashauri ya Mji wa Ruangwa kusaidia kituo cha Walemavu cha Nandaga kwa kupeleka matunzo yote yanayostahili kwa Watu wanaoishi katika kituo hicho.

 Aidha, Dkt Possi alieleza swala la kusaidia Walemavu hao si suala la Watu fulani kama vile Watu wa Ustawi wa Jamii, Maendeleo ya Jamii au Madaktari, bali ni jukumu la kila Mtu. Dkt. Possi aliyaongea hayo alipotembelea kituo cha Walemavu cha Nandaga