Sunday 12 February 2017

KAMPUNI YA URANEX WAKABIDHI BATI 266 KWA AJILI YA UJENZI WA SHULE MPYA WILANI RUANGWA

Na: Mwanakheri Ally

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ruangwa Ndugu Andrea Chezue ametoa shukurani kwa Kampuni ya Uranex inayojishughulisha na uchimbaji wa madini aina ya bunyu katika Wilaya ya Ruangwa kwa msaada wa bati waliotoa.

Mkurugenzi amepokea bati 266 kutoka kwa Uranex ambazo zitatumika katika kuwekeza madarasa matano na vyoo ambavyo vinajengwa katika shule ya sekondari mpya inayojengwa kwa nguvu za Wananchi, Halmshauri na misaada kutoka kwa wadau mbalimbali.

Aliyasema hayo wakati akipokea bati hizo kutoka kwa Meneja wa Uranes Mamboleo walipokuwa wanamkabidhi siku ya tarehe 11-02-2017 katika eneo la kiwanda cha kukamulia mafuta ya ufuta mjini Ruangwa.

Pia alisema Mkurugenzi "ujenzi wa vyumba vya madarasa umefikia katika hatua nzuri na unaenda kama ambavyo ilikuwa inategemewa na kesho wanaanza kupaua na kupiga mbao" aidha, aliwaomba Uranex waendelee na moyo huo huo wa kuweza kusaidia katika maeneo mengine wanatakapoombwa msaada.

''Tangu tumeanza ujenzi wa shule hii mpya Uranex tumekuwa nao bega kwa bega kwani walikuwa wanakwenda mara kwa mara kupitia katika eneo la ujenzi kuona hali ya kiujenzi inavyoendelea'' alisema.

Kampuni ya Uranex ilitoa msaada wa bati 266 kama ahadi waliyoitoa katika Ziara ya kikazi ya  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alivyokuja mwezi wa Disemba mwaka 2016 ilyofanyika katika Wilaya ya Ruangwa

Naye Mkuu wa Wilaya Joseph Mkrikiti aliwaomba wadau wengine ambao hawajatoa ahadi walizoahidi basi waweze kutoa ili kuweza kufanikisha ujenzi huo kuisha mapema na Watoto waliokosa nafasi katika shule ya Ruanngwa Sekondari waanze masomo katika shule hiyo mpya.

Aidha, aliuomba Uongozi wa Halmshauri kutunza rasilimali wanazopewa kwa ajili ya ujenzi ili isiwavunje moyo wanaotoa misaada hiyo na kumuomba Mkurugenzi kuwa makini na matumizi ya vifaa hivyo vinavyotolewa na Watu.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya aliuomba Uongozi wa kampuni ya Uranex kutokuwachoka pale wanapokuiwa wanaitaji msaada kwani wao ni Watu wanaowategemea kufanya Ruangwa kuwa Ruangwa ya maendeleo.

Baada ya kupokea Msaada huo Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi na timu ya Wataalamu walioongozana nao waliweza kutembelea shule hiyo inayojengwa na uwanja wa mpira wa Nyasi bandia unaotegemea kujengwa Ruangwa mjini.


Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri na Wataalamu kutoka ofisa ya Mkuu wa Wilaya na wengine kutoka kampuni ya Uranex wakiwa wamesimama wanamsubiri Mkuu wa Wilaya afike katika eneo la tukio

Meneja wa Uranex Aizaki Mamboleo akiwa anaonesha mzigo wa bati walizozileta kama msaada kwa ajili ya kuezekea vyumba vya madarasa  katika shule mpya

(katikati )Meneji wa Uranex  akiwa na (kulia) Mkurugenzi Mtendaji) Andrea Chezue (kushoto)Mkuu wa Wilaya wakiwa katika eneo la tukio la kupokea bati.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ruangwa Andrea Chezue akiwa anatoa shukurani kwa kampuni ya uranex kwa moyo waliouonesha wa kutoa msaada wa bati hizo

Meneja Uranex akiwa anamkabidhi Mkuu wa Wilaya bati walizoleta kwa ajili ya ujenzi wa vymba vya madarasa na choo katika shule mpya.
Mkuu wa Wilaya Joseph Mkirikiti akiwa anamkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Andrea Chezue bati aliyozabidhiwa na Meneja wa Uranex

Mkuu wa Wilaya akiwa anaongea na watu waliohuidhuria katika tukio hilo baada ya kupokea bati 266 kutoka katika kampuni ya uranex(kushoto kwake) Katibu Tawala Haji na( kulia) Mkurugenzi Mtendaji Andrea Chezue

Wataalamu kutoka Halmshauri ya Wilaya ya Ruangwa wakiwa wanamsikiliza Mkurugenzi Mtendaji akitoa shukurani zake kwa kampuni ya uranex
Vyumba vya madarasa ambavyo vinategemewa kuanza kupauliwa na ndiyo vyumba vitakavyowekwa bati zilizotolewa na uranex



Mkuu wa Wilaya Joseph Mkirikiti akiwa anaongea na Mkurugenzi Andrea chaezue na wataalamu wengine katika eneo la shule mpya



Mafundi katika eneo la shule wakiwa wanatengeneza mbao kwa ajili ya kupandisha kenchi

Mafundi wakiwa wanaendelea na shughuli za kiujenzi ili kuweza kumaliza shughuli hiyo mapema

Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji wakiwa wanakagua matundu ya vyoo katika shule hiyo mpya

Mkurugenzi akiwa anamuuliza fundi Juma kwanini ujenzi wa vyoo umesimama kwa maana hauendani na kasi ya madarasa


Mhandisi wa Ujenzi Nalupi akiwa anatoa maelezo katika uwanja unaotegemewa kujengwa wa nyasi bandia katika Wilaya ya Ruangwa kwa Mkuu wa Wilaya

Mkurugenzi Andrea Chezue akiwa anamapa maelezo Mkuu wa Wilaya Joseph Mkirikiti(Kushoto) na (kulia ) Afisa Mipango Thomas Luambano

Mkurugenzi akiwa anaongea na Meneja wa Uranex Mamboleo (kulia)akimpa maelezo ya uwanja na mambo mengine yanatotegemewa kufanywa na Halmashauri kama kuwa na gadeni

Mkuu wa Wilaya Joseph Mkirikiti akiwa katika picha ya pamoja na watoto wa eneo la dodoma mahali ambapo uwanja unategemea kutengenezwa







MKURUGENZI WILAYA YA RUANGWA AWAHIMIZA WALIMU KUZINGATIA MAADILI YA TAALUMA YAO

Na: Mwanakheri Ally

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Ndugu Andrea Godfrey Chezue amewaaasa Walimu na kuwataka kuwa na nidhamu katika maeneo yao ya kazini na hata nje ya kazini kwani hii itasaidia kuweza kurekebisha nidhamu kwa Wanafunzi wanaowafundisha.

Alisema Mwalimu mwenye nidhamu ni rahisi kumfanya Mwanafunzi anaemfundisha kuwa na nidhamu ambayo itapelekea kuongeza kiwango cha ufaulu katika mitihani ya ndani na nje ya shule.

Hayo ameyaongea wakati wa kikao cha wadau wa elimu kilichohusisha Waratibu Elimu Kata, Wataaluma, Wakuu wa shule na Makamu kilichofanyika katika ukumbi wa Rutesco kikiwa na lengo la kuangalia njia za kuweza kutoka katika hali ya ufaulu wa sasa uliopo na kufikia nafasi nzuri zaidi.

Naye Afisa Utumishi wa Wilaya ya Ruangwa, Festo Mwangalika amewataka Walimu kutenga muda wa kuzungumza na Wanafunzi wanaowafundisha pale ambapo wanakuwa wamewakosea kwani hii inaaweza ikasaidia kubadili mienendo mimbovu ya Wanafunzi.

Pia aliwaambia  Walimu na Waratibu Elimu Kata kuweza kuwafuatilia Wanafunzi wanaowafundisha ili kuweza kubaini wenye tabia mbovu na kuwasaidia mapema kwani hii itasaidia hata kuongeza ufaulu wa Wanafunzi kwani Mwanafunzi mwenye adabu ni rahisi kuwa na maendeleo mazuri.

Naye Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari, Bi. Hawa Mchopa Bi Zena alisema ilikuweza kuongeza kiwango cha ufaulu katika Wilaya ya Ruangwa inatakiwa Wazazi wawape Walimu ushirikiano katika malezi ya Wanafunzi hao ili kuweza kufikia lengo

Kwani  Watoto hawalelewi na Walimu na Wazazi tu , bali malezi ya Moto ni yajamii nzima, hivyo Jamii inatakiwa kutoa ushirikiano katika malezi hii itasaidia kutoka katika eneo moja kwenda eneo jingine katika hali ya ufaulu.

Afisa Taaluma Robert Bujiku wa Halmashauri ya Ruangwa akiwa anafanya utambulisho wa wadau wa elimu hao waliosimama ni waratibu elimu kata 
Afisa Taaluma akiendelea kufanya utambulisho na hao waliosimama ni wakuu wa shule zilizopo katika wilaya ya Ruangwa
Afisa Taaluma akiendelea kutambulisha na hao ni walimu wakuu wasaidizi wa shule za Wilaya ya Ruangwa
Waratibu wa Elimu kata, Wataaluma Wakuu wa Shule na wasakidizi wao wakiwa wanamsikiliza Mkuu wa Wilaya Joseph Mkirikiti
Mkuu wa Wilaya Joseph Mkirikiti akiwa anaongea na wadau wa elimu (kushoto) Afisa Taalum Richard Bujiku (kulia) Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Ruangwa
Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Festo J mwangalika akiwa anaongea na wadau wa elimu katika kuangalia ni jinsi gani wanaweza kuongeza ufaulu wa wanafunzi
Mkuu wa Shule ya Sekondari Likunja Mohammed Lukangaakiwa anatoa maoni yake ya jinsi ya kuongeza ufaulu wa wanafunzi katika Wilaya ya Ruangwa
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mbekenyera Shanly Nchimbi akiwa anawasilisha moani yake ya kwanini ufaulu kwa mwaka huu wilaya ya Ruangwa kwa kidato cha nne umeshuka na nijinsi gani mwakani utaweza kuiongezeka
Wadau wa Elimu na Wataalamu kutoka Halmashauri ya Ruangwa wakiwa wanamsikiliza Mkuu wa shule ya Mbekenyera
Mkuu wa Shule ya Nambilanje Mwl. Kilindo akitoa maoni yake katika kikao cha wadau wa elimu kilichofanyika katika ukimbi wa Rutesco
Mwalimu wa Taaluma katika Shule ya Sekondari Nambilanje Tibazarwa akitoa maoni yake ya kuongeza ufaulu na akizungumza vitu vinavyosababisha kushuka kwa ufaulu.
Naye Mwalimu Mkuu msaidizi wa Shule ya Sekondari ya Ruangwa akitoa changamoto zilizosababisha kushuka kwa kiwango cha ufaulu katika shule hiyo


WANANCHI WILAYA YA RUANGWA WAHIMIZWA KUPANDA MICHE YA MIKOROSHO ILI KUKUZA UCHUMI NA KUHIFADHI MAZINGIRA

Na: Mwanakheri Ally

Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania, Mama Anna Abdallah amewahamasisha Wananchi wa Mji wa Ruangwa kupanda miche ya korosho kwa wingi katika maeneo yao kama ilivyo kampeni ya upandaji miti inayoendelea.

Mwenyekiti wa Bodi hiyo alisema "kwani lengo la kupanda miti  ni kuepukana na jangwa na Watu kuwa na sehemu za kupumzikia hivyo basi ni bora kupanda miti ya korosho kwasababu itamsaidia Mwananchi kupata kivuli na pia kuongeza kipato unapofika muda wa kuvuna korosho hizo".

Aliyasema hayo wakati wa kufanya uziduzi wa kampeni ya kupanda mikorosho mipya 5000 katika kila kijiji kwa msimu wa 2016/2017 katika kijiji cha Chimbila 'B' tarehe 10/02/2017 wakati akiongea na Wananchi wa Kijiji hicho.

Pia aliwataka Wananchi kutumia fursa hiyo ya kuwa na miche mipya na kuipanda katika mashamba yao kwani lengo la kuwa na miche hiyo mipya ni kuongeza uzalishaji wa zao la korosho katika Mkoa wa Lindi.

Naye mgeni Rasmi katika uzinduzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Godfrey Zambi aliwaambia Wakuu wa Wilaya zilizopo ndani ya Mkoa wa Lindi washindane katika kupanda miche hiyo mipya kwani hii italeta manufaa makubwa katika Wilaya hizo kwa kukuwa kiuchumi.

Alisema Mkuu wa Mkoa "inawezekana kufikia malengo ambayo Halmshauri zimejiwekea kama wataweza kuwahamasisha Wananchi wao kupanda miche mipya na kuwasimamia hao wanaokabidhiwa hiyo miche katika kuipanda na kuihudumia mpaka kufikia kipindi cha uvunaji.

Aidha Mkuu wa Mkoa Zambi aliwaambia Wakulima  wanaokabidhiwa miche hiyo ya korosho waweze kuitunza na waisimamie vizuri bila kuangalia kama wamepewa bure au wamenunua kwani kufanya hivyo itasaidia kuongeza uzalishaji katika zao la korosho.

Bodi ya Korosho Tanzania imefanya uzinduzi wa kampeni ya kupanda mikorosho mipya 5000 kila Kijiji katika msimu wa 2016-2017 katika Kijiji  cha Chimbila 'B' ikiwa ni mwanzo wa uzinduzi ambao utafanyika katika Mikoa mingine tena.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe.Godfrey Zambi wa pili kulia akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania Mama Anna Abdallah wa kwanza kulia wakiwa wanasubiri shughuli ya uziduzi ianze
Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania akiwa anaongea na Wananchi wa Kijiji cha Chimbila 'B' wakati wa uziduzi wa kampeni ya kupanda mikorosho mipya 5000, wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa bodi ya korosho Dastani Kaijage na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Godfrey Zambi 

Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi Twaha Mpembenwe akimkaribisha Mgeni Rasmi aweze kuongea na Wananchi wa Chimbila 'B'


Mgeni Rasmi ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Godfrey Zambi akiwa anaongea na Wanakijiji cha Chimbila 'B' na Wataalamu waliohudhulia uzinduzi wa kampeni ya kupanda mikorosho mipya 5000 kila Kijiji


Wanakijiji na Wataalamu kutoka Wilaya za Mkoa wa Lindi wakiwa wanaangalia kikundi cha ngoma kikitumbuiza 

Kikundi cha Ngoma cha Nangumbu Lekatulinge kikiwa kinajiandaa kuingia uwanjani kutumbuiza 

Wapigaji Ngoma wa kikundi cha Lekatulinge wakiwa wanapiga ngoma zao kwa madoido ya kufikisha ujumbe kwa wananchi



Wanakikundi wa Likatulinge wakiwa wanaimba kwa kucheza kwa kufaraha m,bele ya mgeni Rasmi


Mjumbe wa Bodi ya Korosho Edga Maokolo akiwa anatumbuiza mbele ya mgeni rasmi na wageni waalikwa baada ya kupewa nafasi ya kipekee 

Miche ya miti ya korosho 4300 ya kikundi cha jitegemee ikiwa imeoteshwa vizuri na ikiwa tayari kwenda kupandwa katika mashamba

Mohamed Chilambo akiwa anasoma risala mbele ya mgeni rasmi kabla ya kumumkabidhi miche ya korosho
Mama Anna akimkabidhi mche wa mkorosho mkulima Asha kwa ajili ya kwenda kupanda shmabani kwake

Mkuu wa Wilaya akiwa anapokea mche wa mkorosho kutoka kwa Afisa Kilimo Vailet Richard kwa ajili ya kwenda kupanda

Mratibu wa Korosho Richard Bendera akiwa anatoa maelezo kwa wakurugenzi watendaji wa halmashauri ya Ruangwa, Liwale na Kiliwa jinsi ya kupanda mche wa korosho

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ruangwa akiwa anapanda Mche wake wa Mkorosho katika shamba la mkulima lililochaguliwa

Mkurungenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ruangwa akiwa amemaliza kupanda mche aliokabidhiwa


Mwenyekiti wa Manspaa ya Lindi Makwinya na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ruangwa Adrea Chezue wakiwa wamemaliza kupanda mkorosho
Mwenyekiti wa Manspaa ya Lindi  na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ruangwa wakiwa wananawa mikono baada ya kumaliza zoezi la kupanda miti

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Liwale  Justine Monko akiwa anapanda mche aliokabidhiwa

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Liwale akiwa amemaliza kupanda mti wake na akisubiri kuumwagilia maji

Mjumbe wa Bodi ya Korosho Faith Mitambo akiwa anaandaa mche wake wa ajili ya kupanda

Mkurugenzi wa Manspaa ya Lindi akiwa anafanya maandalizi ya kupandikiza Mche aliokabidhiwa kupanda

Mkurugenzi wa Manspaa ya Lindi Jomaary Mrisho Satura akiwa anapanda mche aliokabidhiwa

Mkurugezi wa Manspaa ya Lindi akiwa amaemaliza kupanda miche wake

Afisa Kilimo wa Wilaya ya Ruangwa akiwa anapanda mche wa mkorosho

Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania akiwa ananawa mikono baada ya kumaliza kubanda mti wake