WAZIRI MKUU Kassim
Majaliwa amesema hakuna kijiji nchini kitakachoachwa bila ya kuunganishiwa
umeme katika awamu ya tatu ya Mradi wa Nishati Vijijini (REA).
Amesema Serikali imetenga
shilingi trilioni moja kwa ajili ya kusambaza umeme katika vijiji 8,000 ambavyo
bado havijaunganishiwa nishati hiyo.
Waziri Mkuu alitoa kauli
hiyo jana jioni (Jumanne, Julai 11, 2017) alipozungumza kwa nyakati tofauti na
wananchi wa wilaya ya Ruangwa.
Waziri Mkuu ambaye
ameambatana na mkewe Mama Mary Majaliwa aliyasema hayo katika mikutano
aliyoifanya kwenye vijiji vya Chiapi, Nandanga, Mbecha na Luchelegwa, ikiwa ni
siku ya pili ya ziara yake ya kikazi ya siku nne Mkoani Lindi.
“Rais wetu Dkt. John
Magufuli anajali sana wananchi wake, hivyo ametenga fedha nyingi
zitakazotosheleza kusambaza umeme katika vijiji vyote vikiwemo na wilaya ya
Ruangwa. Gharama za kuunganishiwa umeme huo ni sh. 27,000 tu.”
Pia Waziri Mkuu
amesema mwananchi hawatowajibika tena katika kulipia nguzo wala fomu za
maombi ya kuunganishiwa umeme, kwa sababu tayari gharama hizo zimeshabebwa na
Serikali.
Waziri Mkuu aliongeza
kwamba lengo la Serikali ni kufikisha umeme kwenye vijiji vyote Tanzania
na kwa vile ambavyo viko kwenye maeneo yaliyo mbali na gridi vitafungiwa sola,
jambo ambalo litafungua fursa za ajira na kukuza uchumi.
 |
Waziri Mkuu akisalimiana na Mkuu wa Wilaya Joseph Mkirikiti alipowasili katika kijiji cha Likwachu |
 |
Mkuu wa Wilaya Joseph Mkirikiti akimkaribisha Mkuu wa Mkoa Godfrey Zambi ili aendelee na itifaki nyingine |
 |
Wakazi wa Kijiji cha Likwachu wakiwa wanamsikiliza Waziri Mkuu alipokuwa anazungumza |
 |
Waziri Mkuu akizungumza nawakazi wa kijiji cha Likwachu alipofanya ziara yake katika kijiji cha Likwachu |
 |
Waziri Mkuu akisalimiana na wanakijiji cha Litama alipofika katika kijiji hiko |
 |
Waziri Mkuu akisalimia wananchi alipofanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Ruangwa |
 |
Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa akikagua mradi wa daraja la Likuledi, linalo unganisha
Wilaya ya Ruangwa na Wilaya ya Masasi, kutoka kwa Mhandisi Josam Mlaki, kwenye ziara ya kikazi ya siku nne Mkoani
Lindi |
 |
Waziri Mkuu akifungua Hospitali ya Watu wenye mahitaji maalumu Nandanga alipofanya ziara ya kikazi wilayani humo |
|
|
|
|
|
|
 |
Mbunge wa Liwale Zuberi akiwa anasalimia wakazi wa kijiji cha Likwachu alipopewa nafasi hiyo na Mkuu wa Mkoa |
 |
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Andrea Chezue akiwa anaelezea jinsi watakavyokarabati Zahanati la Likwachu |
 |
Wananchi wakiwa wanamsubiri Waziri Mkuu katika kijiji cha Litama |
 |
Mbunge wa Ndanda Mwmabe akitoa shukurani kwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwapelekea Mradi mkubwa wa kujenga daraja linalounganisha Wilaya ya Ndanda na Ruangwa katika kijiji cha Nandanga kilichopo Wilaya ya Ruangwa |
 |
Mhandisi wa Ujenzi Mashaka Nalupi akipokea maagizo kutoka kwa Waziri Mkuu katika kijiji cha Likwachu |
 |
Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa akiwa anasalimiana na mafundii,wanalojenga daraja linalo
unganisha Wilaya ya Ruangwa na Wilaya ya Masasi,kwenye ziara
ya kikazi ya siku nne Mkoani Lindi, Julai 11, 201 |