Thursday 18 May 2017

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Awataka Wananchi Kumuunga Mkono Waziri Mkuu Katika Kushiriki Shughuli za Maendeleo


NA Mwanakheri Ally

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa ,Mhe, Rashidi Nakumbya amewata wakazi wa Wilaya ya Ruangwa kumuunga mkono Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Kassim Majaliwa.

Amewataka wananchi kufanya kazi bega kwa bega na Mhe, Waziri katika kuleta maendeleo katika wilaya ya Ruangwa kwa Kushiriki shughuli za kimaendeleo alisema,maendeleo katika wilaya hii ni jukumu la kila mkazi wa eneo hili.

Alisema haya wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani lililofanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia Mei 17 mpaka 18 katika ukumbi wa Rutesco mjini Ruangwa.

Mhe, Nakumbya aliwataka waheshimiwa Madiwani wa Wilaya ya Ruangwa kuhakikisha wanatumia nafasi zao katika kuhamasisha wananchi wao katika kuchangia kufanya shughuli za kimaendeleo katika kata zao.

“Nisiwe mchoyo wa kushukuru kama watu wamefanya vizuri basi ni wajibu wangu kuwapa pongezi, nawapongeza wananchi wa kata ya Nachingwea na Ruangwa kwa kazi nzuri ya waliyoifanya ya kujitolea katika ujenzi wa shule ya mpya ya Sekondari Kassim Majaliwa” alisema Mhe, Nakumbya.

Aidha alimtaka Mkurugenzi Mtendaji Andrea Chezue kuongea vizuri na  wachimbaji wa visima waliopo katika wilaya kwa ajili ya kuchimba visima, waanze na shule ya sekondari mpya kwani ikianza bila maji itakuwa shida kwa wanafunzi na walimu.

“Shule yetu ni nzuri sana ila itaendelea kuwa nzuri pale maji yatakapopatikana, maji ni uhai hatuwezi kuanza kutumia shule hiyo bila kuwa na maji kwani  itakuwa mateso kwa watoto wetu wakike pamoja na walimu ” alisema Mhe, Nakumbya.

Pia Mhe, Nakumbya aliwataka wananchi wa wilaya ya Ruangwa kuhakikisha wanasafisha mashamba yao ya mikorosho ili mgao wa dawa ya kupulizia utakapofika  kila Mkulima aweze kupata dawa hiyo na pia alisisitiza itazingatiwa zaidi kwa wale ambao wenye mashamba masafi.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu, Afya na Maji Mhe, Eliasi Nkane aliwaomba wakuu wa shule na Afisa Elimu wa Wilaya kuhakikisha wanafuatilia sheria ya mtoto anayeaacha kwani watoto hawa wasipochukuliwa hatua inasababisha kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi wanaoacha shule.

“Zama za sasa imepunguza sana idadi ya watoto wa mitaani hivyo walimu na maafisa elimu ni wajibu wao kuwachukulia hatua watoto hawa wanaocha masomo ili tuzidi kutokomeza suala la watoto wa mtaani” alisema mhe Nkane.

                              


(kushoto)Diwani wa kata ya Namichiga Mikidadi Mbute akiwa anasikiliza Mwenyekiti wa Halmashauri akizungumza na (kulia) Diwani wa viti maalumu


Mhe, Diwani wa kata ya Mbwemkuru Selemani Likuche akiwa anawasilisha taarifa ya kata yake

Mganga Mkuu wa Wilaya Dr, Japheti Simeo akiwa anajibu hoja

Wataalamu kutoka halmashauri wakiwa wanasikiliza uwasilishwaji wa taarifa za kata na Madiwani

Wakuu wa idara na vitengo wakiwa wanasikiliza uwasilishwaji wa tarifa

Waheshimiwa Madiwani wakiwa wanafuatilia kwa umakini mkutano wa Baraza

Mhe, Diwani wa kata ya Luchelegewa Jaffari Chande akiuliza swali kwa Mkurugenzi Mtendaji


Waheshimiwa wakiwa wanasikiliza kwa umakini Mkutano  ukinaendelea

(katikati)Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Rashidi Nakumbiya (kulia kwake) Makamu mwenyekiti wa Halmashauri Shabani na kushoto kwake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri

Mkuu wa Idara ya Fedha Frank Chonya akiwa anajibu hoja iliyoulizwa na Mhe, Diwani



Diwani wa Viti Maalum Paulina Mmuya akiwasilisha Taarifa ya kata ya Nachingwea

Diwani wa kata ya Ruangwa Mhe, Omari Pendeka akiwasilisha taarifa ya kata yake

Afisa Elimu Sekondari Bihuria Shabani akijibu hoja iliyouliza


Mhe, Diwani wa Viti Maalumu Amina Naenje akiwasilisha taarifa ya kata ya Mnacho

kushoto) Mwandishi wa Mkutano Bashiri Kauchumbe akiwa anafuatilia mkutano unavyoendelea

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Lawrence Mapunda akijibu hoja iliyotoka kwa Mhe, Diwani


Mwenyekiti wa Halmashauri akitoa ufafanuzi kwa wajumbe na waheshimiwa Madiwani


Wajumbe waliohudhuria Mkutano wa Baraza la Madiwani wakifuatilia mjadala iliyokuwa inaendelea


(kushoto) Mkuu wa kitengo cha Ukaguzi wa Ndani na kulia kwake mkuu wa idara ya Mipango


Kiamu Mkuu wa Kitengo cha Sheria Moses Mkwesela akitoa ufafanuzi wa vifungu vya sheria


Diwani wa kata ya Nandagala  Chikongwe akiuliza swali wakati wa kipindi cha maswali na majibu


Mwenyekiti wa Halmashauri Rashidi Nakumbya akifunga Mkutano wa Baraza