Monday 21 August 2017

NHC Imetoa Msaada Wa Mabati 300 na Saruji 300 Katika Shule Ya Sekondari Kassim Majaaliwa



Na Mwanakheri Ally

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mheshimiwa Joseph Mkirikiti ametoa shukurani kwa Mkurugenzi  wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa msaada wa vifaa vya ujenzi lililoutoa katika shule mpya ya Sekondari ya Kassim Majaliwa iliyopo Ruangwa Mjini.

Shirika la Nyumba la Taifa limetoa msaada wa bati 300 na mifuko ya saruji 300 katika shule mpya ya Kassim Majaliwa ikiwa ni kwa lengo la kuanza ujenzi wa Maabara shuleni hapo.

Mheshimiwa Mkirikiti aliliomba shirika hilo lisichoke kutoa msaada kwani shule hiyo bado ni changa na ina mahitaji mengi ya miundo mbinu ambayo hayajakamilika kujengwa pia alilitoa hofu kwa kusema kuwa vifaa vilivyotolewa vitatumika kama inavyotakiwa.

“Tunataka shule hii iwe ni shule ya mfano katika Mkoa wa Lindi hivyo vifaa vilivyotolewa tutavitumia vizuri katika kujenga miundombinu yenye hadhi inayohitajika ili kuifanya shule hii kuwa imara na ya kudumu”, alisema Mh,Mkirikiti.


Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri Thomas Luambano akiongea na Meneja wa (NHC) Gibson Mwaigomole katika Shule ya Sekondari Kassim Majaliwa
kushoto) Meneja wa (NHC) Mkoa Gibson Mwaigomole(kulia)Mkuu wa Wilaya Joseph Mkirikiti  wakiwa katika chumba cha makabidhiano ya msaada uliotolewa na (NHC)


kushoto) Meneja wa (NHC) Mkoa Gibson Mwaigomole(katikati)Mkuu wa Wilaya Joseph Mkirikiti na( kulia) ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Thomas Luambano wakiwa katika chumba cha makabidhiano ya msaada uliotolewa na (NHC) na (wamwisho) Katibu Tawala wa Wilaya Twaha Mpembenwe

Meneja NHC akikabidhi bati kwa Mkuu wa Wilaya katika Shule ya Sekondari Kassim Majaliwa walipoenda kutoa msaada

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa akipokea mifuko ya saruji 300 kutoka kwa Shirika la Nyumba la Taifa

kushoto) Meneja wa (NHC) Mkoa Gibson Mwaigomole(katikati)Mkuu wa Wilaya Joseph Mkirikiti na( kulia) ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Thomas Luambano wakiwa katika chumba cha makabidhiano ya msaada uliotolewa na (NHC)

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mhe, Joseph Mkirikiti akitoa neno la shukurani baada ya kupokea msaada kutoka kwa Shirika la Nyumba la Taifa(NHC)