Wednesday 19 July 2017

Kamati ya Huduma za Jamii Imetembelea na Kukagua Miradi ya Maendeleo


Na Mwandishi Wetu

Kamati ya Afya, Elimu na Maji imefanya  Ziara ya kutembelea   na Kukagua  Miradi ya Maendeleo ya Halmashauri ya Wilaya ikiwa ni utekelezaji wake kila robo ya mwaka.

 kamati hiii iligawanyika katika makundi mawili kundi A na B makundi hayo yalifanya ziara hiyo siku ya tarehe 19/7/2017 kundi A liliongozwa na  Mwenyekiti wa Kamati Mhe Eliasi Nkane , na Kundi B liLiongozwa na Mhe  wa Kamati  akiambatana na wajumbe.

Kamati ilitembelea Miradi  ambayo ni Mradi wa kuona shule ya awali  , kata ya  Nangurugai, Kisima cha Maji , Mihewe , Ujenzi wa Zahanati, Namtatila, , ,Kuona Ujenzi wa vyumba vya madarasa Nambilanje, kuona ujenzi wa Zahanati Chikundi.

Kupitia Ziara hii Mhe Mwenyekiti Eliasi Nkane aliwataka wananchi waendelee kujitolea katika kufanya shughuli za kimaendeleo katika kata zao na kuacha kutegemea kila jambo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri,alisema kijiji kitakachoanzisha mradi kitapewa kipaumbele cha kusaidiwa.

"Halmashauri inamipango mingi ya kimaendeleo kukaa kusubiri yenyewe ndiyo ijekuwaanzishia miradi ni kujichelewesha, tumieni fursa zenu vizuri katika kuanzisha miradi kwani serikali ya Wilaya ipo pamoja na nyie"alisema Nkane

Kaimu Afisa Elimu Kifu akitoa maelezo katika shule ya awali iliyojengwa kwa nguvu za wananchi.
(kulia)Diwani wa kata ya Mbwemkuru Mhe Likuche na( kushoto) wakiwa wanasikiliza maelezo kutoka kwa Kaimu Afisa Elimu Msingi


Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii akiwa anaangalia mazingira ya shule ya awali iliyojengwa kwa nguvu za wananchi

Mazingira ya Nje ya chumba kinachohifadhi mitambo ya kusafishia maji kijiji cha Mihewe


Mitambo ya kusafishia maji iliyopo katika kijiji cha Mihewe

Mwenyekiti wa Kamati akiwa anasikiliza taarifa kutoka kwa Fundi Sanifu Maji Ng"itu

Katikati Mganga Mkuu wa Wilaya Dr Japhet Simeo(kulia) Kaimu Afisa Elimu wakiwa wanaangalia jengo la Zahanati ya Namtatila

(kushoto) Mhe Diwani ya Kata ya Mandawa na (kulia) Mhe Diwani wa kata ya Ruangwa Hassani Pendeka wakiwa wanasikiliza Mwenyekiti wa Kijiji Cha Namtatila akisoma Taarifa ya Zahanati wanayojenga

Waheshimiwa Madiwani wa viti Maalumu wakiwa wanasikilia taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Namtatila

Serikali ya Kijiji ikiwa katika jengo la Zahanati ya ikitoa maelezo juu ya ujenzi huo

Jengo la Zahanati ya Namtatila lililojengwa kwa nguvu za Wananchi mpaka kufikia hapo

Vyumba viwili vya madarasa katika shule ya msingi Nambilanje vilivyojengwa kwa nguvu za wananchi na kushirikiana na Halmashauri

Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Nambilanje Charles Chitawala akiwa anasoma taarifa kwa wanakamati ya huduma za jamii

Mwenyekiti wa Kijiji cha Chikundi Issa Rashidi akitoa maelezo ya Zahanati

Mtendaji wa kijiji cha Chikundi akisoma taarifa ya ujenzi kwa wanakamati ya Afya, Elimu na Maji


Jengo la Zahanati ya Chikundi lililojengwa kwa nguvu za wananchi mpaka kufikia hapo