Wednesday 19 April 2017

KATIBU TAWALA AWAASA WANASACCOS KUFANYA MAREJESHO YA MKOPO KWA WAKATI



NA MWANAKHERI ALLY

Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi Ramadhani Kaswa amewataka wanavikundi wa saccos wanaokopa kutoka katika mfuko wa halmashauri kuweza kurejesha mkopo wao kwa wakati.

Alisema kuweza kufanya hivyo kwa wakati itasaidia kuwapa nafasi vikundi vingine kuweza kukopa na kubadili kiwango cha maisha kutokana na biashara watakazokuwa wanafanya.

Ameyasema hayo wakati akiongea na kikundi cha vijana saccos mjini Ruangwa alipokuwa katika ziara ya kikazi ya kutembelea maendeleo miradi ya Halmashauri.

Aidha alisema ni vyema wahasibu wa kwenye saccos wapewe mafunzo ya kuweza kuendesha mifumo ya utunzaji fedhana vitabu vya kifedha ili waweze kuandesha saccos zao kitaalamu zaidi na itasaidia kuwa na umakini katika suala za kifedha.

Wakati huo huo Katibu Tawala alitoa pongezi kwa uongozi wa Wilaya kwa ujumla kwa kufanikiwa kujenga shule mpya kwa wakati mfupi na kwa kuzingatia viwango na ubora vya kiufundi

‘’Mazingira ya shule ni mazuri kwa mwanafunzi kupatia elimu ila mafundi zidisheni kasi ili shule iweze kumalizika mapema na wanafunzi waanze kutumia majengo yao”alisema

Pia alimtaka Mhandisi wa Maji kufikiria mbinu za kuweza kuwasaidia Shule ya Sekondari Mbekenyera ili waweze kupata jenereta lao la kutumia kupampu maji katika kisima.


jengo la ofisi ya Mkuu wa wilaya lililopo katika hatua za ukamilishaji


Katibu Tawala Ramadhani Kaswa akiwa anakagua jengo jipya la ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Ruangwa

Katibu Tawala akiangalia ujenzi ulipofikia wa jengo la ofisi ya Mkuu wa wilaya Joseph Mkirikiti

Katibu Tawala(katikati)  na msafara wake wakiwa  katika shule mpya iliyopo kata ya Nachingwea

Wanafunzi wakiwa wanafanya usafi katika maeneo ya shule mpya


Wanafunzi wa kidato cha kwanza wanaotegemewa kuhamia katika shule hiyo mpya wakiwa wanasafisha mazingira


Wanafunzi wakiwa wanapanda maua mbele ya vyumba vya madarasa

Muonekano wa vyumba vitatu vya madarasa katika shule mpya inayoitwa Kassim Majaliwa

Mtambo wa kusafishi maji uliopo katika kijiji cha Mihewe kilichopo katika Wilaya ya Ruangwa


(Kulia)Mhandisi wa Maji wa Wilaya Lawrence Mapunda akiwa anatoa maelezo kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi alipotembelea mradi wa maji katika kijiji cha Mihewe


k(kushoto katibu Tawala akiwa anaongea anaangalia eneo lililojengwa jengo kisima cha kuchujia maji(kulia)Afisa Elimu wa Wilaya Bihuria Shabani

(katikati)kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri akiwa anamuonesha(kushoto) Katibu tawala tanki lililojengwa katika kijiji cha mihewe

Tanki la kuhifadhia maji lililojengwa katika kijiji cha Mihewe lenye ujazo wa lita elf 25


Chumba cha darasa kilichopo katika shule ya Mbekenyera High school

Katibu tawala Ramadhani Kaswa akiwa anaongea na wataalamu kutoka Halmashauri na walimu katika shule ya sekondari Mbekenyera

Baadhi ya wakuu wa Idara mbalimbali wakiwa wanasikiliz risala inayosomwa na mwalimu mkuu wa shule hiyo


Mkuu wa Shule ya Mbekenyera akiwa anasoma risala mbele ya katibu tawala wa mkoa wa lindi Ramadhani Kaswa


(kushoto)Katibu tawala akiwa ameongozana na kaimu Mkurungenzi wakielekea katika vyumba vya madarasa katika shule ya msingi Namilema

Katibu tawala akiwa anaangalia mradi wa vyumba vya madarasa Namilema

Wakuu wa idara wakiwa na Katibu Tawala wakiangalia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya msingi Mbekenyera